FAIDA YA KUJUA NJIA YA KUPATA WOKOVU

Namna gani tunaokolewa ? Je nikwa kazi ambazo tunafanya ?

MATANDA SDA

6/24/20252 min temps de lecture

Mnamo fundisho la pili tuliona kwamba mwanadamu alikataa maagizo ya Mungu na kujiletea magumu, hata na kifo cha milele. Ila, tuliona pia kwamba, Mungu hakumuachilia katika hali hiyo, bali alimuahidia mkombozi ambaye ni Yesu Kristo.

Katika fundisho letu la leo, tutaona namna, mwanadamu anaweza kumuendea Yesu na kupata wokovu.

Kwa kupata wokovu, mwanadamu anapiga hatua tatu maishani mwake:

1) Mtu anapokea wokovu kwa neema (kwa bure), anapo kuwa angali mwenye dhambi: Warumi 5:6-8,10; Waefeso 2:8,9.

Hadisi ya mwanamke mzinifu (Maria, dada wa Lazaro). Yohana 8:1-11; Luka 17:11-19 (wakoma kumi).

2) Neema ya Mungu inavutia mutu kwa Yesu

Baada ya kuponywa hukumu la wayahudi, Maria alivutwa na neema ile ya Yesu. Tangu wakati huo, alipenda awe karibu ya Yesu. (Yohane 12:1-8); Luka 7:36-38; Yohane 12:32 “Nami kama nikinyanyuliwa juu ya dunia, nitakokota watu wote kwangu.”

Mmoja wa wakoma kumi, alipo ona ameponywa, alirudi kumutukuza Yesu (Luka 17:15).

Mfano wa mwalimu aliye kuja kushukuru mwongozi wa shule kwa uvumilivu alio muonyesha kazini. Yohana 3:16; Luka 19:10.

3) Neema hiyo inawezesha mutu kuishi maisha ya kumpendeza Mungu na kumutukuza

Maria alipo ona ameponywa kwa neema, hakuendelesha tabia ya uzinifu. Alijuwa kwamba, jambo hilo lingeweza kuhuzunisha rafiki wake aliye muponya kifo cha wa Yuda. Hivyo akaishi maisha ya kumutukuza Yesu. Na kwa kuonyesha furaha yake akafanyia Yesu kitendo cha kumuonyesha shukrani. Luka 7:37,38; Luka 7:47-50 (ona pia shukrani ya mkoma; Luka 17:15,17,18,19 “Imani yako imekuokoa”.

Mfano wa Maria na mkoma, unatufundisha ginsi tunapaswa kufikiria wokovu wetu. Tunapo kumbuka hali yetu ya dhambi, tulikuwa watu wa kupotea milele. Lakini, Yesu kwa upendo wake, alikubali kuchukua hiyo laana yetu na akafa kwa nafasi yetu.kwa upendo wake, ametimiza jambo hilo na tungali wenye dhambi.

Sasa leo, tunapo tambua wokovu ule ambao tumepewa kwa neema, tunaalikwa kuja kwa Yesu, na, kuishi maisha yanayo mpendeza.

2Wakorinto 5:14 : « Maana mapendo ya Kristo yana tulazimisha sisi »

Yohane 14:15: “Kama mukinipenda mutatii amri zangu”

1Yohane 4:19: “Sisi tunapenda kwa maana yeye alitupenda sisi kwanza”

Soma pia 1Yohane 5:3; 2:4

Hatushiki amri ili tuokolewe; bali kwa sababu tumekwisha kukolewa kwa neema, tunavutwa na ule upendo wa mwokozi kumupendeza tukishika amri zake. Tito 2:11-14

MWITO: Wale wote wanao shukuru Mungu kwa wokovu aliowatolea kwa neema kupitia Yesu Kristo, na ambao wana ahidi kuonyesha shukrani hiyo wakifanya mapenzi yake, atawawezesha kutimiza ahadi hiyo. « Kumbukeni kwamba siri ya kupata wokovu kamili ni kumjua Mungu na kufanya mapenzi yake »