FAIDA YA KUJUA JINSI MWANADAMU ALIVYO INGIA MAGUMUNI

Kwanini tunateseka siku za maisha ? Namna gani tunaweza kupata suluhisho kwa magumu haya ya Ulimwengu huu ?

Matanda-SDA/Bienveillant

6/23/20253 min temps de lecture

brown concrete building under starry night
brown concrete building under starry night

Tunapo soma katika kitabu cha mwanzo sura ya 1 na ya 2; Biblia ina tuonyesha namna mwanadamu ameumbwa tofauti na viumbe vingine. Mungu alimuumba kwa mfano wake, na akamupa madaraka ya kutawala viumbe vingine. Lakini baadaye, hali ya maisha ya mwanadamu, ilipaswa kutokana na uamuzi wake wa kutii au kuasi maagizo ya Mugu. Hii inamaanisha kwamba, mwanadamu angeweza kuendelea na maisha ya furaha ikiwa tu angekubali kutii maagizo ya Mungu. Na wakati angelizarau maagizo haya, basi alipaswa kuingia katika magumu. Leo tutajifunza nukta zifuatazo:

1. Hali ya mwanadamu kabla hajatenda dhambi:

- Wakati dhambi ilikuwa haijaingia ulimwenguni, mwanadamu alikuwa katika mazingira mazuri sana. (Mwanzo 1 :31)

- Wazazi wetu waliumbwa kwa mfano wa Mungu (Mwanzo 1 :26-27)

- Walipewa utawala juu ya viumbe vingine (Mwanzo 1 :28)

- Walipewa chakula kizuri na kinacho watosha kwa maisha yao (Mwanzo 1:29, 2:8,9a

Mungu aliwajulisha shurti waliyo paswa kutimiza ili maisha yao yaendelee kuwa ya furaha. Lakini, walikuwa huru kukubali shurti hiyo au kuikataa. Mwanzo 2:15-17

2. Hali ya mwanadamu alipo kwisha kutenda dhambi

Kabla hatuja ingia kwa undani wa nukta hii, tuone kwanza kama dhambi ni nini? (Yohana 3:4). “Kila mtu anaye tenda dhambi, anafanya uasi; kwa kuwa dhambi ni uasi.”

Wazazi wetu walipaswa kuhesabiwa waaminifu na watiifu, wakati wote wangekuwa wanashika maagizo ya Mungu. Lakini, walipo yazarau na kutenda kinyume nayo, hivyo walionekana kwamba wao ni waasi, na wenye dhambi, kwa sababu “dhambi ni uasi”

a. Uamzi mbaya: Mwanzo 3:5,6

b. Hatari ya tamaa na kiburi: Mwanzo 3:6-8

Shetani alianza kwa kuingiza mashaka juu ya neno la Mungu. Alipokwisha kuvuta Hawa (Eva), akashitaki Muumbaji kwamba alisema uongo, na kama alipenda kubakiana neema ambayo angeweza kutolea viumbe vyake. Alisema:

“Hakika hamutakufa”

“Macho yenu yatafungujliwa”, na

“Muta kuwa kama Mungu mukijua uzuri na ubaya”

Kosa la Adamu na Hawa lilikuwa la kujipenda wenyewe kuliko Mungu. Dhambi ya uchoyo imeonekana kwa watu wengi. Moyo wa uchoyo ni moyo wa tamaa na kiburi.

3. Matukio ya dhambi

Mwanadamu alipotenda dhambi, matukio mabaya yalikuwa mengi. Magumu yalimufikia.

a. Kifo kilijitokeza (Mwanzo 2:17; Waroma 6:23a), “Kwa maana mushahara wa dhambi ni mauti, …”;

b. Uhusiano kati ya wazazi wetu uliharibika: Mwanzo 3:12 (Linganisha na Mwanzo 2:23);

c. Uhusiano wao na Mungu uliharibika: Mwanzo 3:8-11 (Linganisha na Mwanzo 1:26-28);

d. Walitambua kama wanavaa uchi: Mwanzo 3:10;

e. Dunia ililaaniwa sababu ya dhambi: udongo haukomalishe mimea tena; miiba ilijitokeza;

f. Kazi ya mikono ikakuwa ya kuchokesha, hata na kwa wakati fulani, bila kuleta faida: Mwanzo 3:17, 18.

g. Mwanamke atazaa kwa uchungu: Mwanzo 3:16;

h. Mchoko wa kiakili na kimwili

i. Magonjwa ya aina mbalimbali, ulemavu na shida zingine vilikumba wanadamu na viumbe vingine

- Ajali zinazo leta ulemavu

- Watoto wanaozaliwa bila viungo fulani vya mwili.

j. Dhambi ikaenea duniani pote: Romain 5:12

k. Dhambi iliharibu mfano wa Mungu ndani ya mwanadamu : Warumi 5 :19 ; Zaburi 51 :7 ; Yobu 14 :4.

Leo mwanadamu anaogopewa na wenzake kuliko kuogopa hata mnyama.

4. Upendo wa Mungu kwa mwanadamu aliye tenda dhambi.

Wakati wazazi wetu walipochagua kifo, hakungekuwa tena tumaini la maisha. Kifo hiki kilikuwa cha milele. Lakini, Mungu kwa upendo wake mwingi, alionyesha huruma kwa mwanadamu. Mwanzo 3:7, 21,15.

Shahili hili la 15 ni la ahadi yenye faraja kubwa.

Ahadi hii ili husu Yesu aliye paswa kuja kuokoa wanadamu. Shetani angeweza muponda kisingino (tazama mateso na shida shetani alizo letea Yesu na anaendelea kwa watu wake), lakini Yesu yeye angemuponda kichwa. Ushindi wa Yesu juu ya shetani ni ushindi juu ya dhambi.

Yesu ashukuriwe kwa sababu amepata ushindi kamili juu ya shetani (Yohana 19 :30 ; Matayo 28 :18). Kazi ya Yesu ya kuokowa wanadamu, inatupatia tumaini la kushinda dhambi na kupata uzima wa milele.

MWITO: Kiisha kutenda dhambi, tulikuwa watu wa kufa milele. Lakini Mungu alitayarisha njia ya kutuponyesha. Je unaweza muambia Mungu, aksante kwa yale uliyo nitendea, nina kutolea maisha yangu ili uyatawale ? Mungu akubariki.

Barikiwa na video hii hapo chini.