FAIDA YA KUJUA NI NINI KINACHO TOKEA BAADA YA KIFO

Watu wa moja wanafikiri kwamba baada ya kifo maisha yanaendelea. Wengine wanapoteza tumaini na kufikiri kwamba mtu akiisha kufa hawezi kuishi tena. Je, Biblia ina sema nini kuhusu hali ya wafu?

HOME COMING

Matanda SDA/Bienveillant

7/1/20251 min temps de lecture

Watu wa moja wanafikiri kwamba baada ya kifo maisha yanaendelea. Wengine wanapoteza tumaini na kufikiri kwamba mtu akiisha kufa hawezi kuishi tena. Je, Biblia ina sema nini kuhusu hali ya wafu?

Katika fundisho letu tutaona yafuatayo:

1) Kifo ni nini?

- Kabla ya kujibu kwa swali hili, hebu tuone kwanza namna mwanadamu alivyo umbwa. Mwanzo 2:7: Uhai wa mtu ni MAVUMBI+PUMZI YA UHAI; Mwanzo 3:19 na Zaburi 146:3, 4: Mavumbi yanapo tengana na pumzi ya uhai, mtu haishi tena. Anaitwa maiti. Hivi, kifo kinakuwepo wakati vitu hivi viwili vimetengana.

- Mavumbi yanaenda wapi? Mwanzo 3:19

- Pumzi ya uhai inaenda wapi? Mhubiri 12:7, 3:19-21.

Roho inayo rudi kwa Mungu si mtu, bali ni pumzi (souffle). Hii inakuwa kama courant ambayo inarudi pahali ilipotoka wanapo funga iterupteur, ampoule inapozimika. Hivyo courant si ampoule, bali ina saidia ampoule kuwaka.

2) Wafu wako wapi, na wanaweza fanya kitu gani?

- Yohana 5:28,29: wafu wako makaburini

- Wafu hawajui kitu: Mhubiri 9:5,6; Zaburi 6:5; Yesaya 38:10-11

- Shetani na malaika wake wanadanganya watu: 2Wakorinto 11:13,14

- Wafu wote (waamini na waovu, wapo makaburini; hakuna anayeenda mbinguni. Wote wanangojea siku za ufufuo).

Wafu wataishi tena?

- Kifo kinalinganishwa na usingizi: Yohana 11:11

- Wafu watafufuliwa: Yohane 5:29; Danieli 12:1-2; 1Watesalonika 4:13-18

- Wakati wa matengenezo: Mhubiri 9:10

SWALI: Nani anaye jua tarehe yake ya kufa?

Namna tumekwisha kusikia, kifo ni hakika. Wakati wa kutengeneza maisha yetu ni leo, tunapo kuwa tungali hai. Baada ya kifo hakuna uwezo wa kufanya jambo Fulani.

MWITO: Je, unaelewaje upendo wa Mungu hata kama kifo kingali duniani ? Unaweza kujitoa kwa Yesu kabla kifo hakija kufikia? Ungependa kumwamini Yesu kusudi, hata kama utakuwa umelala, uweze kufufuka na kuishi milele? Aksante.